Video musicale
Video musicale
Crediti
PERFORMING ARTISTS
Stamina Shorwebwenzi
Performer
COMPOSITION & LYRICS
BONVENTURE ELIUTER KABOGO
Songwriter
PAUL TIMOTH MWASILE
Songwriter
PRODUCTION & ENGINEERING
PAUL TIMOTH MWASILE
Producer
Independent artist
Producer
TML
Producer
Testi
Intro
Wamemchokoza tena bwana….
Wamemchokoza bear……….
Umeskini niache..…eeh! eeh! Eeh! x3
Verse 1
Aah!..Ulimuondoa mama kipindi yupo hoi anaumwa/
Akapoteza uhai kisa pesa ya matibabu hakuna/
Wewe ndio sababu ya kuvunja ndoa ya Fatuma/
Mumewe mambo mazito haujampa pesa umeuchuna/
Niache niende bwana nimechoshwa na Maisha huku sitimbi/
Unadhani sitamani kupiga picha kidimbwi/
Nizungushe wapambe mezani tungi jingi/
Mixer kuagiza vinywaji vijavyo na cheche nyingiii/
Umeniganda aisee,umeniganda kama ruba/
Hivi we ni jinsia gani, hiv ni pisi ama mjuba/
Unanichanganya kuna muda nautamani msuba/
Unanizeesha,unanikondosha sasa si unipe tu hizo fuba/
We ndiyo sababu ya dada zangu wakae kona wanajiuza/
Na Kaka zangu wawe wezi huko buza/
Na mama zangu wakeshe kuuza vitumbumbua /
Unawatesa baba zangu kuwazugusha kwenye jua/
Chorus
Usione tabasamu usoni moyoni mimi sina furaha (eeh)
Usione napendeza nje,ndani mimi nakufa na njaa
Umaskini niache,niache,niache…. X2
Verse 2
Nimesoma kidumu ufagio Kayumba ndio nako weza/
Hivi unadhani sitamani Watoto wangu wasome fedha/
Daily kwa mganga napiga manyanga/
Nazi njia panda,ili mladi tu niweza kuupata huo mkwanja/
Nikuulize nikiwa Tajiri inakuuma nini/
Au navyoitwa mbahiri kiongozi unapata nini/
Kaka zangu bodaboda nao utawapa pesa lini/
Iseeh,tumechoka kubet tutaliwa mpaka lini/
Kwenye mapenzi,wengi tupo tu ilimradi/
Ukiitwa mpenzi na hauna pesa wewe ni mpenzi mtazamaji/
Au unafurahi nikiitwa dume suruali/
Dume nisiye na gari ,dume nisiye na maisha ya ufahari /
Mbona wenzangu unawapa marolls royce ,maprado/
Mimi nikiendesha ujue naharisha ,mbona kwangu mambo bado /
Inatosha iseeh,hembu niache niende zangu/
Nipate utajiri nikakae na maboss wenzangu/
Chorus
Usione tabasamu usoni moyoni mimi sina furaha (eeh)
Usione napendeza nje,ndani mimi nakufa na njaa
Umaskini niache,niache,niache…. X2
Verse 3
watoto wa shangazi bado ni wahudumu wa bar/
hawapendi wanachofanya sema ndio hivyo tu wana njaa/
na mjomba wangu bado ni mkataa mkaa /
mtoto wake fundi mwashi mjenzi wa majengo ya mtaa/
hivi kwa nini kazi ngumu zote za sisi maskini/
unatuona power mabula eeh!!! Dah!
Hivi kwa nini/
Maisha wanayoishi yote tunayaunda sisi/
Mijengo magari mpaka hayo maofisi/
Nachukia nikiona sura ya mbunge wangu/
Nawaambia haki ya nani nimepoteza kura yangu/
Anasinzia bungeni hatetei Maisha yangu/
Bora peke yangu mimi pekee na fuvu langu/
Chorus
Usione tabasamu usoni moyoni mimi sina furaha (eeh)
Usione napendeza nje,ndani mimi nakufa na njaa
Umaskini niache,niache,niache…. X2
Hook
Nimekuchokaaah x3
Nimekuchoka umaskini
Nimechoka……aaah
Written by: BONVENTURE ELIUTER KABOGO, PAUL TIMOTH MWASILE


