Ambassadors of Christ Choir 熱門歌曲
積分
出演艺人
Ambassadors of Christ Choir
表演者
作曲和作词
Ambassadors of Christ Choir
作曲
歌詞
Mtu mmoja alistaajabu sana, niliposema nitamshukuru Mungu
Baada ya matatizo mengi kunipata akili yangu ikampa wasiwasi
Kwa kweli nami, ilinigharimu, kujijulisha inipasavyo
Ila baada ya muda nikaona yapo mengi ya kunifanya nimshukuru Mungu
Yako mengi, hayajakwisha yatubidhishayo tumshukuru Mungu wetu
Japo twapita majaribu mengi bado, yapo mengi ya kushukuriwa
(Jiunge), he, ee, jiunge nasi, tulisisitize jambo hili la muhimu
Yale yote tujiulizayo mioyoni majibu anayo Mungu wetu
Ambassadors of Christ tuashukuru lakini kwa wengi hatueleweki
Kutokana na mambo ya yaliotupata ivi kushukuru si jambo la busara
Lakini ndugu (eh), ukitulia, nakujiuliza ya ajali ile
Tungeweza kuangamia wote kwa pamoja asiwepo hata mmoja wa kusimulia
Yako mengi, hayajakwisha yatubidhishayo tumshukuru Mungu wetu
Japo twapita majaribu mengi bado, yapo mengi ya kushukuriwa
(Shukuru), he, ee, jiunge nasi, tulisisitize jambo hili la muhimu
Yale yote tujiulizayo mioyoni majibu anayo Mungu wetu
Majaribu kama haya yalikuweko hata kwenye siku za mababu zetu
Ila kwa yote walikuwepo mashujaa walioweza kuitetea imani yao
Tuwake Mungu (eh), wakati wote, kwa yote hatujitegemei
Tukiwa hai tukiwa mauti tuwake tujualo ni moja kushukuru
Yako mengi, hayajakwisha yatubidhishayo tumshukuru Mungu wetu
Japo twapita majaribu mengi bado, yapo mengi ya kushukuriwa
(Jiunge), he, ee, jiunge nasi, tulisisitize jambo hili la muhimu
Yale yote tujiulizayo mioyoni majibu anayo Mungu wetu
He ee jiunge nasi, tulisisitize jambo hili la muhimu
Yale yote tujiulizayo mioyoni majibu anayo Mungu wetu
Writer(s): Ambassadors Of Christ Choir
Lyrics powered by www.musixmatch.com