Lyrics

Salamu nimezipata ulotuma kunambia Salamu nimezipata ulotuma kunambia Nasikia wajinata Leo utanitambia Lakini utanikuta Sabaha nakungojea Lakini utanikuta sabaha nakungojea Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Wewe kuku wewe kuku chakula chako jaani Wewe kuku wewe kuku chakula chako jaani Mimi njia mimi njiwa huletewa mikononii Kama hujui uliza mimi nawe bora nani Kama hujui uliza mimi nawe bora nani Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Mahali ukichukizia huzuka kila mazuo Mahali ukichukiza huzuka kila mazuo Huzidi na miujiza kusudi uvunjwe cheo Japo wajipendekeza katu huwi mtu kwao Japo wajipendekeza katu huwi mtu kwao Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Ni bure hamunipati mbio mukaniendea Ni bure hamunipati mbio mukaniendea Mtakufa na laiti uku mkinishuhudia Nimewashinda bahati ndipo mkanichukia Nimewashinda bahati ndipo mkanichukia Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Dunia yetu ya leo si ya watu kusemana Dunia yetu ya leo si ya watu kusemana Kila alie na lake aombe Rabbi salama Kama langu limetota na lako wewe litazama Kama langu limetota na lako wewe litazama Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Mtu akitaka sema kwanza hutizama lake Mtu akitaka sema kwanza hutizama lake Akazunguka na nyuma kutizama yalokwake Hainuki kusimama kutangaza ya mwenzake Hainuki kusimama kutangaza ya mwenzake Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Mwafanya muyatakayo mimi sisemi ya mtu Mwafanya muyatakayo mimi sisemi ya mtu Yangu yafata mbio komeni roho za kutu Kwanza safisheni nyoyo kisha mseme ya watu Kwanza safisheni nyoyo kisha mseme ya watu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Sijali mimi sijali maovu mkinitangaza Sijali mimi sijali maovu mkinitangaza Ni mambo tangu akali si mwanzo kujitokeza Najua msema kweli kwa wengine huchukiza Najua msema kweli kwa wengine huchukiza Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Nina neno ndugu zangu nawaeleza sikizeni Nina neno ndugu zangu nawaeleza sikizeni Kutangwa jina langu kwa uzushi mtaani Hamnitii machunguu walakwangu si magenii Hamnitii machunguu walakwangu si magenii Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Ukitaka jenga nyumba ukajengee mjini Ukitaka jenga nyumba ukajengee mjini Nadirisha na dirisha ulielekeze kusini Hauna nywele kichwani sasa chanuo la nini Hauna nywele kichwani sasa chanuo la nini Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe jamaa mwapita mwanilaumu Munani nami viumbe mwapita mwanilaumu
Writer(s): Sabah Salum Lyrics powered by www.musixmatch.com
instagramSharePathic_arrow_out