Credits
COMPOSITION & LYRICS
Edward's Bryan Okoth
Songwriter
Lyrics
[Verse 1]
Sijawai penda kupanda ndege
Hakuna kitu kitafanya nizoee
Nina hofia urefu sio siri
Ninatetemeka nikisafiri
[Verse 2]
Lakini hii kazi nimechagua
Najua itabidi nitembee
Mara nyingi itaturusha
Pande tofauti za dunia
[PreChorus]
Ikifanyika, simu nitachukua
Ili nisikize wimbo
Inirudishe kando yako
Na nitakupigia, sauti nikisikia
Nitajihisi niko kwako
Ukinihitaji hapo
Nitakukumbusha
[Chorus]
Unaweza cheza wimbo wetu
Cheza ni wimbo wetu
Ukinihitaji we' icheze
Wakati wowote
Cheza wimbo wetu
Cheza wimbo wetu
Hata nikiwa mbali aje
Nitakuwa na wewe
[Bridge]
Kwa wimbo wetuu
Huu ni wimbo wetuu
[Verse 3]
Nakumbuka usiku juzi-juzi
Umelala kando yako mpenzi
Nafasi ni kubwa kitandani
Umechagua pande yangu lakini
[Verse 4]
Na Nikikuangalia
Jinsi umetulia
Nilijazwa na raha hii ni baraka
Sanaa
Nikajipata, karatasi nachukua
Nikuandikie wimbo
Nikuanikie roho
[PreChorus]
Ukiamka, afathali utajua
Nakupa penzi dabo-dabo
Ukinihitaji hapo
Nitakukumbusha
[Chorus]
Unaweza cheza wimbo wetu
Cheza wimbo wetu
Ukinihitaji we' icheze
Wakati wowote
Cheza wimbo wetu
Cheza wimbo wetu
Hata nikiwa mbali aje
Nitakuwa na wewe
Kwa wimbo wetu
[Bridge]
Uu-uuh
[Verse 5]
Ukihitaji
Nikuwe nawe
Wewe icheze-icheze
[Chorus]
Ooh, wetu
Cheza wimbo wetu
Ukinihitaji we' icheze
Wakati wowote
Cheza wimbo wetu
Cheza wimbo wetu
Hata nikiwa mbali aje
Nitakuwa na wewe
Kwa wimbo wetu
Huu ni wimbo wetuu
[Outro]
Uuh
Uuh
Written by: Edward's Bryan Okoth