制作

出演艺人
Christina Shusho
Christina Shusho
表演者
作曲和作词
Christina Shusho
Christina Shusho
作曲

歌词

[Verse 1]
Naona pendo kubwa mno latoka kwa Mwokozi wangu
Niteleka na maji mengi yatembeayo baharini
Lanitolea tumaini
Ya kwamba nitatiwa nguvu
Na niwe mhodari tena
Kwa pendo kubwa la Mwokozi
[Verse 2]
Lanitolea tumaini
Ya kwamba nitatiwa nguvu
Na niwe mhodari tena
Kwa pendo kubwa la Mwokozi
[Chorus]
Hallelujah ni pendo kubwa
Linalotoka moyo wako
Ee Mungu wangu nakuomba
Nijaze pendo lako tele
[Chorus]
Hallelujah ni pendo kubwa
Linalotoka moyo wako
Ee Mungu wangu nakuomba
Nijaze pendo lako tele
[Verse 3]
Na pendo hilo kubwa mno
Huyaondoa majivuno
Na kunifunza haki kweli
Uongo wote niuvue
[Verse 4]
Hunituliza moyo wangu
Huruma nayo hunitia
Na sote tuwe na umoja
Katika pendo la Mwokozi
[Verse 5]
Hunituliza moyo wangu
Huruma nayo hunitia
Na sote tuwe na umoja
Katika pendo la Mwokozi
[Chorus]
Hallelujah ni pendo kubwa
Linalotoka moyo wako
Ee Mungu wangu nakuomba
Nijaze pendo lako tele
[Chorus]
Hallelujah ni pendo kubwa
Linalotoka moyo wako
Ee Mungu wangu nakuomba
Nijaze pendo lako tele
[Verse 6]
Nijazwe pendo hilo kubwa
Inibidiishe siku zote
Rohoni niwe na jukumu
Nimtumikie Bwana Yesu
[Verse 7]
Hazina yako nipeleke
Kwa watu waliopotea
Wafahamishwe pendo kubwa
Ulilonalo Mungu wangu
[Verse 8]
Hazina yako nipeleke
Kwa watu waliopotea
Wafahamishwe pendo kubwa
Ulilonalo Mungu wangu
[Chorus]
Hallelujah ni pendo kubwa
Linalotoka moyo wako
Ee Mungu wangu nakuomba
Nijaze pendo lako tele
[Chorus]
Hallelujah ni pendo kubwa
Linalotoka moyo wako
Ee Mungu wangu nakuomba
Nijaze pendo lako tele
Written by: Christina Shusho
instagramSharePathic_arrow_out

Loading...