Music Video

Credits

PERFORMING ARTISTS
Joel Lwaga
Joel Lwaga
Performer
COMPOSITION & LYRICS
Joel Lwaga
Joel Lwaga
Arranger
PRODUCTION & ENGINEERING
Joel Lwaga
Joel Lwaga
Producer
Transsnet Music Limited
Transsnet Music Limited
Producer

Lyrics

Mkono wako umenishika Fimbo yako yaniongoza Gongo lako lanifariji Umenisitiri umenifanya hodari Uliliona chozi langu la ndani Ukalifuta na kunipa amani Unyonge wangu haukukuweka mbali Ukaniinua na kunipa dhamani Eeh Bwana, wanitazama Baba, baba Mungu usielala Wanitazama, wanitazama Baba, baba Mungu usiechoka Mi ni mboni yako Yesu wee(eeh Baba), Yesu wee Jicho lako Yesu wee(eeh Baba), Yesu wee Mi ni mboni yako Yesu wee(eeh Baba), Yesu wee Jicho lako Yesu wee(eeh Baba), Yesu wee Akili zangu Zilifika mwisho Na kuona Mungu hunitazami Taabuni Na wanadamu Wakapata cha kusema kuwa Mungu wangu hayupo Tena nami Nilipoona ni mwisho Wewe ukatangaza mwanzo Nilipodhani ni pigo Kumbe ni lako kusudio Kilipozidi kilio Wewe ukaleta kicheko Ukadhihirisha kwa macho Wewe ni langu kimbilio Uliliona chozi langu la ndani Ukalifuta na kunipa amani Unyonge wangu haukukuweka mbali Ukaniinua na kunipa dhamani Eeh Bwana, wanitazama Baba, baba Mungu usielala Wanitazama, wanitazama Baba, baba Mungu usiechoka Eeh Bwana, wanitazama Baba, baba Mungu usielala Wanitazama, wanitazama Baba, baba Mungu usiechoka Mi ni mboni yako Yesu wee, Yesu wee Jicho lako Yesu wee, Yesu wee Mi ni mboni yako Yesu wee, Yesu wee Jicho lako Yesu wee, Yesu wee Mi ni mboni yako Yesu wee, Yesu wee Jicho lako Yesu wee, Yesu wee Uliliona chozi langu la ndani Ukalifuta na kunipa amani Unyonge wangu haukukuweka mbali Ukaniinua na kunipa dhamani Eeh Bwana
Writer(s): Joel Lwaga Lyrics powered by www.musixmatch.com
instagramSharePathic_arrow_out